Select Menu

Makala

KILIMO BIASHARA

MKULIMA

UFUGAJI

UVUVI

PICHA ZA MAZAO

VIPINDI VYA RADIO

VIPINDI VYA RUNINGA-TV

» » » » HABARI: Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi Mh.Mwigulu Nchemba,amefukuza uongozi wote machinjio ya Ukonga
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

Waziri wa Kilimo na Mifugo Mwigulu Nchemba amefanya ziara ya Kushtukiza saa saba usiku wa kuamikia leo katika Machinjio ya Ukonga Mazizi.

Katika ziara hiyo, Waziri Nchemba  amekamata ng’ombe 200 wakiwa wanaingizwa kwenye machinjio bila kibali halali, na kati yao ni ng’ombe 20 tu ndo walikuwa na kibali cha kuchinjwa, hivyo ushuru  wa ng’ombe 180  ulikuwa  unatafunwa  na  watumishi  waovu.
"Nimekamata ng'ombe 200 wakiwa wanaingizwa kwenye machinjio bila kibali halali, ni ng'ombe 20 tu kati ya hao 200 ndio wanakibali cha kuchinjwa,

Kwa maana hiyo ushuru wa ng'ombe 180 umekwenda mifukoni mwa watumishi waovu na wenye lengo baya dhidi ya serikali yetu.

Hivyo basi, nimewasimamisha kazi kuanzia mkuu wa mnada wa Pugu ambaye siku si nyingi aliaminiwa na serikali na kupewa jukumu ili aongoze mnada huo,watumishi wote waliotajwa kwenye ubadhilifu huo."
Alisema Mwigulu Nchemba 


Baada  ya  kubaini  hali  hiyo,Waziri Nchemba ameufukuza  uongozi wote  wa  machinjio  hayo  na  kuagiza  vyombo  vya  dola  viwakamate  viongozi  wote waliohusika  na  kuwafikisha  mahakamani.

About Agri-business media initiative in Tanzania

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments

Leave a Reply