Pembejeo Bandia Zawaathiri Wakulima Mbeya- Turuka
Serikali ya Tanzania imesema pembejeo hafifu za kilimo wanazouziwa wakulima nchini zimechangia kudidimiza kilimo cha mazo ya chakula nchini na kusababisha kilimo kutokuwa na tija.
Serikali ya Tanzania imesema pembejeo hafifu za kilimo zinazouziwa wakulima nchini zimechangia kudidimiza kilimo cha mazo ya chakula nchini na kusababisha kilimo kutokuwa na tija.
Hayo yameelezwa leo jijini Dar es salaam na Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Chakula na Uvuvi, Dk. Florens Turuka Wakati akizindua mpango wa kuendeleza kilimo kwa wakulima wadogo wa mkoani Mbeya,
Akizindua Mpango huo unaowezeshwa na Serikali ya Norway Dk.Turuka amesema serikali itachukua hatua kwa Makampuni yanayouza pembejeo bandia zisizokidhi viwango katika sekta ya kilimo na kuchangia kudorora kwa uzalishaji wa mazao
Mpango huo umelenga kuwafikia wakulima 30,000 katika mkoa wa mbeya Ifikapo 2020 kupitia Taasisi ya Mapinduzi ya Kijani Barani Afrika AGRA,ambapo serikali ya Norway ilitoa Dola za kimarekani Bilioni 1.2 katika mpango wa awamu ya kwanza.
Kwa upande wake ,Naibu Waziri wa Mambo ya nje ya Norway Tony Skogen amesema serikali yake imelenga kumuinua mkulima mdogo ili kunufaika na kilimo na kuboresha maisha.
Nae Rais wa AGRA,Dkt.Agnes Kalibata anasema katika kila wanawake kumi saba wanategemea kilimo katika kumu maisha yao katika maeneo ya vijijini licha ya changamoto zinazowakabili.
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe.Abbas Kandoro anasema wakulima nchini wa mazao ya chakula wanakabiliwa na changamoto nyingi ikiwa ni pamoja kutofika kwa Pembejeo za kilimo kwa wakati,ukosefu wa mbolea.
No comments